Tuesday, June 27, 2017

HABARI NA PICHA: MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BWENI LA WASICHANA MWANZI SEKONDARI

Na. Mwl. Venance, F. 

Mwenge wa Uhuru leo tarehe 27/06/2017 umetua katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni. Katika moja ya miradi iliyozinduliwa na kuwekea jiwe la msingi katika halmashauri hii ni pamoja na Ujenzi wa Bweni la Wasichana shuleni hapa. Mkuu wa shule Mama Janeth Lubasi akisoma taarifa fupi mbele ya Kiongozi wa mbia za mwenge Bw. Amour Hamad Amour, alisema kuwa, ujenzi wa bweni hilo ulianza tangu mwaka 2010. Uendelezaji wake uliendelea baada ya kuungua kwa bweni la wasichana shuleni hapo. Aidha Mkuu huyo wa Shule aliongeza  kuwa, mradi huo unajengwa kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali, ikiwemo Halmashauri ya Manyoni, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Wafanyabiashara wa Manyoni pamoja na nguvu za wananchi wa Manyoni. Mkuu wa Shule alisema kuwa mradi  ukikamilika utaweza kubeba jumla ya wanafunzi 50 kwa wakati mmoja.  

Aidha Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Bw. Amour Hamad Amour mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi husika. Alimpongeza Mkuu wa Shule, Mkandarasi na wadau wote waliofanikisha mradi huu tena kwa kiwango bora.  Akimuelekea Mkuu wa Shule, Kiongozi huyo wa mbio za mwenge alisema, "Hongera sana mama...yaani hapa umepata Hosteli. Mimi nimeukubali kwa asilimia mia." aidha alimtaka mkuu huyo wa shule kuwahimiza wanafunzi wasome kwa bidii, wafundishwe uzalendo na kuijua nchi yao.

Hapa chini nimekuwekea picha za tukio zima..... 

Mkuu wa Shule akisoma taarifa ya mradi
 Mkuu wa Shule akiusubiri Mwenge wa Uhuru

Burudani za ngoma za asili zilikuwepo

Wazee wa matarumbeta pia walikuwepo kutumbuiza

 Bweni la wasichana linalojengwa




 



















Habari na picha na Mwl. Venance, F.
0715 33 55 58/0755 44 06 99

Tuesday, May 9, 2017

MATUKIO KATIKA PICHA: WAHITIMU WA KIDATO CHA VI 2017 MWANZI SEC. WAWAAGA WALIMU WAO KIAINA

Na. Mwl. Venance F.
Wanafunzi wa kidato cha sita 2017 mara baada ya kumaliza mtihani wao wa mwisho leo (Jumanne, tar. 9/5/2017) waliamua kuwashukuru na kuwaaga walimu wao. Walimu walitoa nasaha mbalimbali kwa wahitimu hao zoezi lilioenda sambamba na wanafunzi kuwalisha keki walimu wao kama ishara ya shukrani lakini pia Mkuu wa shule kwa niaba ya walimu wote aliwalisha keki wahitimu hao kama ishara ya kuwatakia mema na kukubari shukrani yao. Nimekuwekea hapa picha zinazoeleza tukio zima:

 Wanafunzi wa Kidato cha Sita 2017 wakiwa wamekusanyika
 katika ofisi ya Mkuu wa Shule kusikiliza nasaha za mwisho
 kabla ya kutawanyika kuelekea mtaani

 Afande nae akaamua kutwanga foto na wanafunzi
 alioshiriki kuwasimamia


 Mkuu wa Shule Madam, Lubasi pamoja na afande Lucy 
wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi




 Mkuu wa Shule akiwa katika picha ya pamoja
 na baadhi ya wahitimu kidato cha VI 2017 

 Wahitimu waliandaa keki kwa ajili ya kupongezana na 
kuwashukuru walimu wao


 Mkuu wa Shule Madam Lubasi na Makamu mkuu
 wa shule wakikata keki kwa pamoja huku wahitimu 
wakishuhudia zoezi hilo kwa umakini

Mhitimu akiikatakata keki katika vipande vidogovidogo

Picha zinazofuata ni baadhi ya walimu wakilishwa keki na wanafunzi wao








Picha zinazofuata Mkuu wa Shule akiwalisha keki wanafunzi wake





Kwa jinsi keki ilivyokuwa tamu 
Mkuu wa Shule aliamua kujilisha keki mwenyewe


Mkuu wa Shule kwa niaba ya jumuia ya wana Mwanzi Sec. anawatakia wahitmu hawa kila la heri na kuwataka wawe mabalozi wazuri wa Mwanzi Sec. popote waendapo.
Imeletwa kwenu na Mwalimu Furaha Venance
Mkuu wa idara ya Mawasiliano na Masomo ya Kompyuta (ICS)
Anapatikana kwa namba 0715335558 / 0755440699 
instagram: @fullraha17
HAYA NDIYO MATOKEO YAO YA KIDATO CHA SITA BAADA YA KUTANGAZWA