Wednesday, July 17, 2019

MAKAMU MKUU WA MWANZI SEKONDARI ATEULIWA KUWA MKUU WA SHULE YA ITIGI SEKONDARI

SECOND MASTER
Na. Mwl.Venance, F.
Aliyekuwa Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwanzi, Jacob Mwabeza (pichani) ameteuliwa kuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Itigi iliyopo katika Halmashauri ya Itigi Mkoani Singida. Uteuzi huo umefanyika kujaza nafasi iliyoachwa wazi baada ya aliyekuwa Mkuu wa shule hiyo, Ndugu, Kansheba kuteuliwa kuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwenge iliyopo Singida Mjini.

Mkuu wa shule amemteua Mwl. Sylvery Rashid kuwa Makamu Mkuu wa Shule kuziba nafasi hiyo.

Mkuu wa Shule ya Mwanzi, pamoja na jumuiya ya Mwanzi Sekondari wanampongeza na kumtakia kila la heri Mwl. Mwabeza katika majukumu yake hayo mapya. 


No comments:

Post a Comment