Wednesday, July 17, 2019

MAKAMU MKUU WA MWANZI SEKONDARI ATEULIWA KUWA MKUU WA SHULE YA ITIGI SEKONDARI

SECOND MASTER
Na. Mwl.Venance, F.
Aliyekuwa Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwanzi, Jacob Mwabeza (pichani) ameteuliwa kuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Itigi iliyopo katika Halmashauri ya Itigi Mkoani Singida. Uteuzi huo umefanyika kujaza nafasi iliyoachwa wazi baada ya aliyekuwa Mkuu wa shule hiyo, Ndugu, Kansheba kuteuliwa kuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwenge iliyopo Singida Mjini.

Mkuu wa shule amemteua Mwl. Sylvery Rashid kuwa Makamu Mkuu wa Shule kuziba nafasi hiyo.

Mkuu wa Shule ya Mwanzi, pamoja na jumuiya ya Mwanzi Sekondari wanampongeza na kumtakia kila la heri Mwl. Mwabeza katika majukumu yake hayo mapya. 


Wednesday, June 12, 2019

JOINING INSTRUCTIONS KIDATO CHA V 2019 MWANZI SEC. HII HAPA


HALMASHAURI YA WILAYA YA MANYONI
SHULE YA SEKONDARI MWANZI
 Shule ya Sekondari Mwanzi iko umbali wa Kilometa moja na nusu (1.5 km) Kaskazini Mashariki mwa halmashauri ya  Wilaya ya Manyoni.Muhula wa masomo unaanza tarehe 08/07/2019.  Hivyo Mwanafunzi anatakiwa kuripoti shuleni tarehe
06/07/2019 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 22/07/2019.
 Ingia katika link hapa chini kupata fomu ya maelekezo:

JOINING INSTRUCTIONS KIDATO CHA V 2019 MWANZI SEC BOFYA HAPA