Tuesday, October 29, 2013

Matokeo ya wanafunzi wa sekondari yataanza kupangwa kwa kutumia COURSE WORK zao!

Kamishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalalusesa ameliambia gazeti la Habari Leo kuwa Serikali itabadili mfumo wa upangaji alama za ufaulu wa mitihani ya Sekondari ili kazi anazofanya mwanafunzi shuleni, zitumike katika kumpatia alama ya ufaulu katika mtihani wa mwisho, mfumo unaolandana na ule unaotumika katika Vyuo Vikuu.
 
 
Tayari Serikali imetuma dokezo, ambalo lipo katika tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa wadau wa elimu ili kupata maoni yao kabla ya kuanzisha mfumo huo. Dodoso hilo limeeleza kuwa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995, imeelekeza kwamba katika kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi wa elimu ya sekondari, Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi zitachangia asilimia hamsini na mtihani wa mwisho utachangia asilimia hamsini pia.
 
 
Mathalani, kwa mtihani wenye alama za jumla ya 100, mwanafunzi akipata alama 50 kupitia kazi za shule, atatakiwa kutafuta alama 50 katika mtihani wa mwisho.
 
 
Kwa kutumia mfumo huu, mwanafunzi atakuwa anakwenda kufanya mtihani akiwa tayari anajua alama za mchango wa kazi shuleni (continuous assessment) na kuwa na hakika ya anachotakiwa kukipata wakati anakwenda kufanya katika mtihani:
 
 
“Hatutaki kuona mwanafunzi hanufaiki na kile alichokivuna akiwa shule. Mfano mfumo wa sasa mwanafunzi aliyepata alama F ni aliyepata alama kati ya 0-34"
 
Chanzo: Habari Leo

Sunday, October 20, 2013

MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE 2013 MWANZI SEC.

Wahitimu wa Kidato cha nne 2013 wakiingia ukumbini
 
Wahitimu kidato cha nne 2013 wakiwa wakijiandaa kuketi
 
Mkuu wa Shule, Mwl. Ntiruka akiwatambulisha na
kuwakaribisha wageni
 
Wanafunzi wa kidato cha tano Mwanzi Sec. wakitoa buradani 
 
Wanafunzi wa kidato cha kwanza wakifanya Comedy

Wahitimu wakisoma risala mbele ya mgeni Rasmi
 

 
Wahitimu wakiwafuatilia wenzao wakisoma risala

Wahitimu wakitoa burudani

 Vijana wakishusha mistari ya nguvu
 

Wanafunzi wa kidato cha tatu wakishusha burudani ya kufa mtu
 

Mgeni rasmi, kaimu Mkurugenzi Mzee Masumbuko
akitoa hotuba yake
 
Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani

Mwanafunzi wa kidato cha pili akichukua zawadi
kwa kufanya vizuri darasani

Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani
 
Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani
 
Muhitimu wa kidato cha nne akitunukiwa cheti chake
 
Wahitimu wakiimba shairi

Mmoja wa wahitimu akiwa pamoja na mama yake akionesha cheti
 

  
Mambo ya zawadi na keki hayo
 
Diwani Masabuni wa pili kushoto na viongozi wengine
wakipata msosi
 
 
Imeandaliwa na Mwalimu Venance F.
 

Tuesday, October 1, 2013

HALI ILIVYOKUWA KATIKA KIKAO CHA WAZAZI MWANZI SEKONDARI


Mwl. Venance F.
Leo katika Shule yetu ya Mwanzi, tulikuwa na kikao na wazazi wa watoto wanaosoma shule hii, lengo lilikuwa kukajadili maendeleo ya watoto wao, ya kitaaluma, nidhamu, utotoro na mengineyo, miongoni mwa waliohudhuria ukiachana na walimu wa Mwanzi, ni pamoja na Afisa Elimu Sekondari, Katibu CCM wilaya, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa, Afisa Mtendaji Kata, Mwenyekiti wa bodi, na mjumbe wa bodi, wazazi waliazimia mambo mengi, miongoni mwa maazimio yalikuwa ni, wazazi kuchangia chakula ili watoto wao wawe wanapata chakula hapa shuleni, wazazi kuchangia ujenzi wa bweni [kumalizia bweni lililopo ambalo limefikia kwenye linta]  na uzio wa shule, [hili ni mpango wa muda mrefu], kuchangia ujenzi wa maabara chumba kimoja,  pia watoto wanaokabiliwa na mitihani ya taifa kuweka kambi shuleni, utaratibu uandaliwe wazazi wafaamishwe namna ya kuchangia, watoto wa kike waliopanga mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu shule iangalie namna ya kuwasaidia kukaa shuleni.
kiufupi, kikao kilikwenda vizuri sana, kama ulikosa hayo ndo baadhi ya yaliyokubaliwa na wazazi wa watoto, hivyo tazama picha zifuatazo kujionea hali halisi ya kikao:
Wazazi waliohudhuria kikao
                              Meza kuu, kutoka kushoto, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa,
                                     Katibu Wilaya CCM, Afisa Elimu Sekondari Wilaya,
                                 Mkuu wa Shule, Mwenyekiti wa bodi, Afisa Mtendaji Kata,
                                                                    mjumbe wa bodi

Ktibu wa Wilaya CCM, akijitambulisha

                                                        Afisa mtendaji Kata akichangia

                                               Mwenyekiti wa bodi, akifafanua jambo

 Mzazi akichangia
Kutoka kushoto, Katibu CCM Wilaya,
Afisa Elimu Sekondari na Mkuu wa Shule
wakisikiliza kwa makini





                                                                   Mzazi akichangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                                                  Mzazi akichangia


                                                     Mzazi akiendelea kuchangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                              Mjumbe wa bodi, Mch. Elisante Mwinyigoha
                                                                     akichangia jambo


                                              Afisa Elimu Sekondari akisisitiza jambo

                                                    Wazazi wakiendelea kuchangia

Mwenyekiti wa bodi, ambaye ndiye alikuwa
 mwenyekiti wa kikao akihairisha kikao

 UONGOZI WA SHULE UNAWASHUKURU WAZAZI  NA VIONGOZI WOTE WALIOHUDHURIA KIKAO HIKI, TUNAOMBA TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA KUIJENGA SHULE YETU NA KUINUA TAALUMA YA WATOTO WETU


Thursday, September 26, 2013


HALMASHAURI YA WILAYA YA MANYONI

SHULE YA SEKONDARI MWANZI

 

TANGAZO LA KIKAO CHA WAZAZI

 
Shule ya Sekondari Mwanzi inapenda kuwatangazia wazazi wote wenye watoto wao wanaosoma Shule ya Sekondari Mwanzi kuwa, siku ya jumanne tarehe 01/10/2013 kutakuwa na kikao cha wazazi na wafanya kazi wa shule hii kwa ajili ya kujadili maendeleo ya shule na wanafunzi wa Mwanzi.


Hivyo wazazi wote wenye watoto katika shule hii, mnaombwa kuhudhuria bila kukosa, tushirikiane kwa pamoja namna ya kuinua taaluma ya shule yetu na watoto wetu.

 
Ukiliona tangazo hili, wajulishe na wenzako

Limetolewa na,

…………………………….

E. Ntiruka

MKUU WA SHULE

Wednesday, September 4, 2013

WALIMU WA MWANZI WAAGA WAFANYAKAZI WENZAO, AMBAO WAMEHAMA

 
Na. Mwl. Venance F.
 
Jana Tarehe 03/09/2013, walimu wa Mwanzi, wamefanya Sherehe fupi kuwaaga walimu wa mazoezi pamoja na walimu na wafanyakazi wasiowalimu, ambao wamehamia sehemu mbalimbali, walimu waliogwa ni pamoja na Mwl. Nyakigha, aliyekuwa Mwalimu wa Nidhamu, ambaye amehamia Musoma kuwa Afisa Takwimu na Vielelezo [Sekondari], Mwalimu Shukia aliyekuwa Mkuu wa Shule, ambaye amehamia Singida shule ya Sekondari Mwenge, Fundi Jimmy Mhamiji aliyeamia Tabora Boys, na Muhasibu Philipo S. aliyeamia Dodoma, Manispaa, zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo la kuwaaga wenzetu:
 
 
Kutoka kushoto, Mkuu wa Shule, Ntiruka, akiwa na
waagwa,Jimmy Mhamiji na Mwl.Nyakigha
 
Mkuu wa Shule akitoa neno
 
Fundi Jimmy naye akitoa neno
 
Mwalimu Nyakigha naye akitoa yake ya moyoni
 
 Unamjua huyu! ndiyo Dj. Lubasi
 
Aliyemwakilisha Mkuu wa Shule aliyehama, ndugu Shukia
 
Hapa inaelekea mambo yalikuwa safi, huyo ndo white mwenyewe,
 mwalimu Luka ambaye alikuwa mwenyekiti wa sherehe.
 
Muda wa zawadi huo!!!!!!
 
Walimu hao wakipeleka zawadi
 
Makamu mkuu, akimkabidhi zawadi Fundi Jimmy
 
Mwalimu Deborah akimkabidhi zawadi mwalimu Nyakigha
ambaye amehamia Musoma
 
Hapo mi sitii neno
 
Mwl, Jane Mwaigonela, akikabidhi zawadi kwa
mkuu wa shule, ambayo aliipokea kwa niaba ya Mhasibu,
Philipo ambaye amehamia Dodoma manispaa
 
Prosper na zawadi walimu wenzake wakimsindikiza
 
 
    Mwalimu Prosper akimkabidhi zawadi, Bwana Inno
ambaye alikuwa akimwakilisha Shukia, ambaye
amehamia Mwenge Sec.
 
JUMUIYA YA WANA MWANZI
INAWATAKIA KILA LA HERI KATIKA KULITUMIKIA TAIFA HUKO MUENDAKO
 
Imeandaliwa na Mwl. Venance.