Tuesday, October 1, 2013

HALI ILIVYOKUWA KATIKA KIKAO CHA WAZAZI MWANZI SEKONDARI


Mwl. Venance F.
Leo katika Shule yetu ya Mwanzi, tulikuwa na kikao na wazazi wa watoto wanaosoma shule hii, lengo lilikuwa kukajadili maendeleo ya watoto wao, ya kitaaluma, nidhamu, utotoro na mengineyo, miongoni mwa waliohudhuria ukiachana na walimu wa Mwanzi, ni pamoja na Afisa Elimu Sekondari, Katibu CCM wilaya, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa, Afisa Mtendaji Kata, Mwenyekiti wa bodi, na mjumbe wa bodi, wazazi waliazimia mambo mengi, miongoni mwa maazimio yalikuwa ni, wazazi kuchangia chakula ili watoto wao wawe wanapata chakula hapa shuleni, wazazi kuchangia ujenzi wa bweni [kumalizia bweni lililopo ambalo limefikia kwenye linta]  na uzio wa shule, [hili ni mpango wa muda mrefu], kuchangia ujenzi wa maabara chumba kimoja,  pia watoto wanaokabiliwa na mitihani ya taifa kuweka kambi shuleni, utaratibu uandaliwe wazazi wafaamishwe namna ya kuchangia, watoto wa kike waliopanga mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu shule iangalie namna ya kuwasaidia kukaa shuleni.
kiufupi, kikao kilikwenda vizuri sana, kama ulikosa hayo ndo baadhi ya yaliyokubaliwa na wazazi wa watoto, hivyo tazama picha zifuatazo kujionea hali halisi ya kikao:
Wazazi waliohudhuria kikao
                              Meza kuu, kutoka kushoto, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa,
                                     Katibu Wilaya CCM, Afisa Elimu Sekondari Wilaya,
                                 Mkuu wa Shule, Mwenyekiti wa bodi, Afisa Mtendaji Kata,
                                                                    mjumbe wa bodi

Ktibu wa Wilaya CCM, akijitambulisha

                                                        Afisa mtendaji Kata akichangia

                                               Mwenyekiti wa bodi, akifafanua jambo

 Mzazi akichangia
Kutoka kushoto, Katibu CCM Wilaya,
Afisa Elimu Sekondari na Mkuu wa Shule
wakisikiliza kwa makini





                                                                   Mzazi akichangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                                                  Mzazi akichangia


                                                     Mzazi akiendelea kuchangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                              Mjumbe wa bodi, Mch. Elisante Mwinyigoha
                                                                     akichangia jambo


                                              Afisa Elimu Sekondari akisisitiza jambo

                                                    Wazazi wakiendelea kuchangia

Mwenyekiti wa bodi, ambaye ndiye alikuwa
 mwenyekiti wa kikao akihairisha kikao

 UONGOZI WA SHULE UNAWASHUKURU WAZAZI  NA VIONGOZI WOTE WALIOHUDHURIA KIKAO HIKI, TUNAOMBA TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA KUIJENGA SHULE YETU NA KUINUA TAALUMA YA WATOTO WETU


No comments:

Post a Comment