Tuesday, February 12, 2013

WANAFUNZI NA WALIMU WA MWANZI SEC. WASAIDIA JAMII KWA KUCHANGIA DAMU

Wanafunzi na walimu wa Shule ya Sekondari Mwanzi wameamua kuisaidia jamii kwa kuamua kuchangia damu ili kusaidia kuokoa maisha ya watu mbalimbali wenye mahitaji ya kuongezewa damu katika hospitali mbalimbali mkoani Singida.  Zoezi hilo la uchangiaji damu limefanyika jana jumanne tarehe 12/02/2013 katika Shule ya sekondari Mwanzi.
 
Zifuatazo ni picha mbalimbali za tukio zima la uchangiaji damu.
 
Wanafunzi wa Mwanzi wakihamasishwa kuchangia damu
 
Mwanafunzi wa kidato cha nne akiangaliwa kama damu yake iko ya kutosha
 
Mwanafunzi wa kidato cha nne akiwa tayari kuchangia damu
kama anavyoonekana
 
Mwl. Deborah Mkombozi Akiulizwa maswali ya hapa na pale huku
mwalimu Lubasi pembeni kwa mbali akisubiri zamu yake ifike
 
Wanafunzi wakiwa tayari wameshatoa damu zao
 
Mwalimu Lubasi akipata vipimo kuangalia mapigo ya moyo n.k
 
Chumba kilichotumika ndo hiki, huku wengine wakijipoza na soda, biskuti
 
 
 
 
Haya sasa! chezea sindano wewe! Mwalimu Lubasi naye alijitolea damu
 
Inapendeza sana pale mwalimu Lubasi pembeni mwanafunzi wake
 
Kazi ya kuendelea kuhamasisha wengine kujitolea damu iliendelea
kufanyika katika bwalo la wanafunzi
 
Damu ambazo zilikuwa tayari zikiwekwa vizuri
 
Mwalimu Venance [Mwenye suti] naye alikuwepo
 kuhakisha mambo yanaenda sawa
 
Mwalimu Moris, Venance, Jenipher na Nyakigha wakihakisha
                     hakuna mwanafunzi anayezagaa nje wakati wengine wakiwa
katika zoezi la kuchangiadamu
 
Tunawapongeza walimu na wanafunzi wote walioshiriki kuchangia damu, kwa kufanya hivi watakuwa wamesaidia sana kuokoa maisha ya watu mbalimbali ambao wanaweza kuwa ni ndugu zetu, jamaa zetu, majirani zetu, wasiokuwa na uwezo na watu wa makundi mbalimbali.

MUNGU AWABARIKI SANA
 
Picha na Habari  imeandaliwa na Mwalimu Venance F.

Friday, February 8, 2013

MAHAFALI YA KLABU YA KISWAHILI TAREHE 17/01/2013

Wahitimu wakisoma risala kwa mgeni rasmi
Mwalimu Venance mwenye shati la mistari mistari
 
 Wahitimu wakiburidisha kwa njia ya maigizo
 
 
Walimu wakifuatilia kwa makini igizo kutoka kushoto ni
Mwl. John Maghway, Venance F na Ginatio M.
 Mgeni rasmi akitoa hotuba kwa wahitimu
 
Picha zifuatazo baadhi ya wahitimu wakitunukiwa vyeti
vya Uanachama na Uongozi wa Klabu
 
 
 
 
Makamu Mwenyekiti wa Klabu, Dorika Isaya akikabidhi Faili
la Klabu kwa Mwalimu Mlezi wa Klabu ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi
katika mahafali hayo
 
 Mwalimu John Maghway akitoa neno kwa niaba ya Idara ya Hesabu
 
Huyu ndiye alikuwa msema chochote [MC]  katika shughuli hiyo
Mmoja wa wahitimi [katikati] akionesha cheti alichotunikiwa
Viongozi wa Klabu katika picha ya pamoja na walimu wao
 
Picha ya pamoja kati ya wahitimu na walimu
 
Hawa walikuwa wanafunzi wanaochukua Geography waliwasindikiza
wenzao wa Kiswahili katika picha ya pamoja na walimu
 
BURUDANI KAMA KAWAIDA HAIKUWA NYUMA

TUNAWATAKIA KILA LA HERI WANAFUNZI WOTE WA KIDATO CHA SITA KATIKA
MTIHANI WAO WANAOENDA KUFANYA SIKU YA JUMATATU TAREHE 11/02/2013