Tuesday, October 29, 2013

Matokeo ya wanafunzi wa sekondari yataanza kupangwa kwa kutumia COURSE WORK zao!

Kamishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalalusesa ameliambia gazeti la Habari Leo kuwa Serikali itabadili mfumo wa upangaji alama za ufaulu wa mitihani ya Sekondari ili kazi anazofanya mwanafunzi shuleni, zitumike katika kumpatia alama ya ufaulu katika mtihani wa mwisho, mfumo unaolandana na ule unaotumika katika Vyuo Vikuu.
 
 
Tayari Serikali imetuma dokezo, ambalo lipo katika tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa wadau wa elimu ili kupata maoni yao kabla ya kuanzisha mfumo huo. Dodoso hilo limeeleza kuwa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995, imeelekeza kwamba katika kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi wa elimu ya sekondari, Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi zitachangia asilimia hamsini na mtihani wa mwisho utachangia asilimia hamsini pia.
 
 
Mathalani, kwa mtihani wenye alama za jumla ya 100, mwanafunzi akipata alama 50 kupitia kazi za shule, atatakiwa kutafuta alama 50 katika mtihani wa mwisho.
 
 
Kwa kutumia mfumo huu, mwanafunzi atakuwa anakwenda kufanya mtihani akiwa tayari anajua alama za mchango wa kazi shuleni (continuous assessment) na kuwa na hakika ya anachotakiwa kukipata wakati anakwenda kufanya katika mtihani:
 
 
“Hatutaki kuona mwanafunzi hanufaiki na kile alichokivuna akiwa shule. Mfano mfumo wa sasa mwanafunzi aliyepata alama F ni aliyepata alama kati ya 0-34"
 
Chanzo: Habari Leo

Sunday, October 20, 2013

MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE 2013 MWANZI SEC.

Wahitimu wa Kidato cha nne 2013 wakiingia ukumbini
 
Wahitimu kidato cha nne 2013 wakiwa wakijiandaa kuketi
 
Mkuu wa Shule, Mwl. Ntiruka akiwatambulisha na
kuwakaribisha wageni
 
Wanafunzi wa kidato cha tano Mwanzi Sec. wakitoa buradani 
 
Wanafunzi wa kidato cha kwanza wakifanya Comedy

Wahitimu wakisoma risala mbele ya mgeni Rasmi
 

 
Wahitimu wakiwafuatilia wenzao wakisoma risala

Wahitimu wakitoa burudani

 Vijana wakishusha mistari ya nguvu
 

Wanafunzi wa kidato cha tatu wakishusha burudani ya kufa mtu
 

Mgeni rasmi, kaimu Mkurugenzi Mzee Masumbuko
akitoa hotuba yake
 
Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani

Mwanafunzi wa kidato cha pili akichukua zawadi
kwa kufanya vizuri darasani

Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani
 
Mwanafunzi akichukua zawadi kwa kufanya vizuri darasani
 
Muhitimu wa kidato cha nne akitunukiwa cheti chake
 
Wahitimu wakiimba shairi

Mmoja wa wahitimu akiwa pamoja na mama yake akionesha cheti
 

  
Mambo ya zawadi na keki hayo
 
Diwani Masabuni wa pili kushoto na viongozi wengine
wakipata msosi
 
 
Imeandaliwa na Mwalimu Venance F.
 

Tuesday, October 1, 2013

HALI ILIVYOKUWA KATIKA KIKAO CHA WAZAZI MWANZI SEKONDARI


Mwl. Venance F.
Leo katika Shule yetu ya Mwanzi, tulikuwa na kikao na wazazi wa watoto wanaosoma shule hii, lengo lilikuwa kukajadili maendeleo ya watoto wao, ya kitaaluma, nidhamu, utotoro na mengineyo, miongoni mwa waliohudhuria ukiachana na walimu wa Mwanzi, ni pamoja na Afisa Elimu Sekondari, Katibu CCM wilaya, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa, Afisa Mtendaji Kata, Mwenyekiti wa bodi, na mjumbe wa bodi, wazazi waliazimia mambo mengi, miongoni mwa maazimio yalikuwa ni, wazazi kuchangia chakula ili watoto wao wawe wanapata chakula hapa shuleni, wazazi kuchangia ujenzi wa bweni [kumalizia bweni lililopo ambalo limefikia kwenye linta]  na uzio wa shule, [hili ni mpango wa muda mrefu], kuchangia ujenzi wa maabara chumba kimoja,  pia watoto wanaokabiliwa na mitihani ya taifa kuweka kambi shuleni, utaratibu uandaliwe wazazi wafaamishwe namna ya kuchangia, watoto wa kike waliopanga mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu shule iangalie namna ya kuwasaidia kukaa shuleni.
kiufupi, kikao kilikwenda vizuri sana, kama ulikosa hayo ndo baadhi ya yaliyokubaliwa na wazazi wa watoto, hivyo tazama picha zifuatazo kujionea hali halisi ya kikao:
Wazazi waliohudhuria kikao
                              Meza kuu, kutoka kushoto, Mratibu Elimu kata, Afisa Tarafa,
                                     Katibu Wilaya CCM, Afisa Elimu Sekondari Wilaya,
                                 Mkuu wa Shule, Mwenyekiti wa bodi, Afisa Mtendaji Kata,
                                                                    mjumbe wa bodi

Ktibu wa Wilaya CCM, akijitambulisha

                                                        Afisa mtendaji Kata akichangia

                                               Mwenyekiti wa bodi, akifafanua jambo

 Mzazi akichangia
Kutoka kushoto, Katibu CCM Wilaya,
Afisa Elimu Sekondari na Mkuu wa Shule
wakisikiliza kwa makini





                                                                   Mzazi akichangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                                                  Mzazi akichangia


                                                     Mzazi akiendelea kuchangia

                                                                    Mzazi akichangia

                                              Mjumbe wa bodi, Mch. Elisante Mwinyigoha
                                                                     akichangia jambo


                                              Afisa Elimu Sekondari akisisitiza jambo

                                                    Wazazi wakiendelea kuchangia

Mwenyekiti wa bodi, ambaye ndiye alikuwa
 mwenyekiti wa kikao akihairisha kikao

 UONGOZI WA SHULE UNAWASHUKURU WAZAZI  NA VIONGOZI WOTE WALIOHUDHURIA KIKAO HIKI, TUNAOMBA TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA KUIJENGA SHULE YETU NA KUINUA TAALUMA YA WATOTO WETU