Thursday, August 14, 2014

MWANZI SEC. KUUMANA NA KILIMATINDE KESHO IJUMAA

Na. Mwl. Venance F.
Moja ya kikosi hatari cha mwanzi kilichocheza
 na Chikuyu Sec. miaka ya nyuma

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanzi kufanya ziara ya kitaaluma na michezo katika shule ya sekondari Kilimatinde, katika Ziara hiyo michezo mbalimbali itachezwa. Mwalimu wa Michezo wa Mwanzi Sekondari, Mwl Mwaigonela akitoa ratiba ya ziara hiyo kwa www.mwanzisec.blogspot.com alisema kuwa kabla ya mechi hizo kucheza kutatanguliwa na mdahalo kati ya wanafunzi wa shule hizo, itafuatiwa na mechi kati ya walimu wa Mwanzi Sec. na walimu wa Kilimatinde Sec. na baadaye kuhitimishwa na mechi za wanafunzi.

Akielezea maandalizi ya ziara hiyo, mwalimu huyo alisema kuwa, taratibu zote zimewekwa sawa, wanafunzi wa Mwanzi wana hali ya kuibuka washindi katika michezo yote iliyopangwa kufanyika, huku walimu nao wakiahidi kuwafundisha soka walimu wenzao wa Kilimatinde.

Mwalimu wa Zamu, Mwalimu Sylvery Hussein akiwatangazia wanafunzi wake aliwataka wakajiandae na safari ya kesho, na pia wasisahau kubeba vifaa vya michezo bila kusahau sahani za chakula chakula kitatolewa huko huko kwa wanafunzi wote ili kuhakikisha Kilimatinde wanapewa dozi za maana.

Mungu ibariki Mwanzi Sec. 

No comments:

Post a Comment